Mbeya City Yamfuta Kocha Mecky Maxime na Benchi Lake Kufuatia Matokeo Mabaya, Klabu ya Mbeya City FC imetangaza rasmi kuachana na kocha mkuu Mecky Maxime kufuatia mwenendo usioridhisha wa timu tangu alipojiunga na kikosi hicho.
Mbeya City Yamfuta Kocha Mecky Maxime na Benchi Lake Kufuatia Matokeo Mabaya
Uamuzi huo pia umehusisha benchi zima la ufundi, ambapo kocha msaidizi Nizar Khalfan pamoja na kocha wa viungo Francis Mkanula wameondoka sambamba na Maxime.

Sababu za Uamuzi
Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya klabu, matokeo mabaya ya hivi karibuni ndiyo yaliyochochea uamuzi huo. Mbeya City imekuwa ikipata ugumu wa kupata ushindi katika mechi za ligi, hali iliyoweka presha kubwa kwa benchi la ufundi.
Mbeya City imechukua hatua kubwa kwa kuachana na kocha Mecky Maxime na benchi lake, ikilenga kubadili mwelekeo wa timu. Sasa macho yanaelekezwa kwa uongozi wa klabu kuona nani atakayeteuliwa kuchukua nafasi hiyo na kama mabadiliko haya yatazaa matokeo chanya.
Pendekezo la Mhariri:
- Yanga Yaifunga Mbeya City 6-0, Yazidi Kuongoza Ligi Kuu NBC
- Simba Kusafiri Kumenyana na Namungo, Maandalizi Yaanza Dar es Salaam
- Bernardo Silva Atangaza Kuondoka Man City Baada ya Miaka 9 ya Mafanikio
- Real Madrid Tayari kwa Msimu Usio na Kombe
- Messi Anunua Klabu ya Daraja la Tano ya Uhispania Cornella